Watoto Yatima is a song in Swahili
Ilitokea hawakupenda
Ndio mzunguko wa maisha
Na kama lingekuwa fungu, wasingechagua
Wanahangaika wanateseka wanapata shida hawana tumaini
Wameshaachwa wako peke yao
Mungu watazame kama Baba yao
Wanakutegemea wewe, wanakutazama Bwana
Kilio wanacholia wanalilia moyoni
Maana hata wakilia nani atawafariji
Mungu uwasaidie uwatie moyo, mzigo uwe mwepesi
Jamii imewasahau wanahangaika hata wakiombaomba wanawafukuza
Wengine wanawatukana kuwaita chokoraa Mungu uwakumbuke
Mungu uwakumbuke
Wakiachwa peke yao ubaki nao
Kaa pamoja nao kwenye baridi Kali
Kavifunge vidonda vya mioyo yao
Kazibe pengo lililo mioyoni mwao, wakumbushe wewe ni Baba na Mama yao
Ayayayah una macho huoni na hata ukiona huoni umuhimu
Jifanye kama umekufa uko kuzima sasa inua macho yako tazama duniani
Watazame wanao wanavyoteseka wanadhurumiwa wananyanyasika
Sasa nyosha mkono wako, uwape chakula
Nenda kawatafutie vya kujifunikaaaa
Unagundua hauwezi maana hauna mwili
Tena hawakuoni, maana ulishakufa
Sasa unawafanya Nini watoto wa marehemu
Mbona unawadhurumu Mali za wazazi waoooo sivyo walivyokuachia ili uwanyanyaseee
Usiwatende ubaya ili usije kutendewa
Hivi una uhakika gani kama ukiondoka utamwachia nani watoto wakooo
Je! Wakija kuwatenda kama utendavyo wewe utajisikiaje?
Je! Hayo utayapenda?
Ayayayayyaah hali zao ni mbaya
Ayayayayyaah hali zao ni mbaya
Tazama walivyopauka wa kwako wanatakata
Tena watupa chakula wao hawana
Wanatamani Baba angekuwepo
Mama angekuwepo wasingepata shida
Hawaelewi Nini kimewatokea
Wanjiona wana mikosi jamii imewasahau
Tuwahurumieni Hawa
Tuwaonyeshe upendo wetu
Wengine kwa kujitetea wakaangukia pabaya
Wamefuata mikumbo wako pabaya
Wengine wametenganishwa na wadogo zao
Wengine wako jela lakini tatizo Nini?
Walijaribu kuokoa maisha yao
Wakaenda kuiba
Wengine wanachomwa moto
Tunawalaumu Bado
Kumbe tatizo tumewasahau
Wananenewa maneno makali
Wanasimangwa Hadi wanauguaaaaaa
Ila wafanyaje wanajikaza
Hawana pa kwenda wanavumilia