song lyrics / Ambwene Mwasongwe / Tangulia Mbele lyrics  | FRen Français

Tangulia Mbele lyrics

Performer Ambwene Mwasongwe

Tangulia Mbele song lyrics by Ambwene Mwasongwe official

Tangulia Mbele is a song in Swahili

Mbele yangu (pita) Bwana (pita) Yesu (pita, mbele yangu pita)
Mbele yangu (pita) pita Bwana (pita) Pita (pita, mbele yangu pita)
Mbele kuna hatari, Mbele kuna maadui, mbele kuna vitisho mbele kuna mashimo
Mbele kuna vita, mbele kuna ugomvi, tangulia mbele
Nikweli nimepanga mambo mengi kufanya lakini usalama wangu umebaki kwako mwenyewe
Ndio maana leo nimekuja, kupiga magoti mbele zako
Ninaomba nisaidie uende mbele yangu,
Macho yangu hayaoni nini kiko mbele ...Natumaini wewe wewe umeona,
Tangulia mbele yangu Bwana kanyooshe mapito
Siwezi kwa ufahamu wangu nataka leo nishinde ii (Kama ukienda mbele yangu hakuna jambo maagumu nitashindwa, nitajiachia kama tai nikijua wewe bwana uko mbele)

Mbele kuna hatari (pita), Mbele kuna maadui (pita), mbele kuna vitisho (pita, mbele yangu pita)
Mbele kuna vitaa (pita) mbele kuna ugomvi (pita), tangulia mbele (pita, mbele yangu pita)
Nikweli nimepanga mambo mengi kufanya lakini usalama wangu umebaki kwako mwenyewe
Mbele kuna hatari, Mbele kuna maadui, mbele kuna vitisho mbele kuna mashimo
Mbele kuna vitaa mbele kuna ugomvi, tangulia mbele
Nikweli nimepanga mambo mengi kufanya lakini usalama wangu umebaki kwako mwenyewe

Nataka kuwa shujaa ...
Bwana nisaidie
Ila ushujaa wangu ni kukutegemea wewe
Najua hakuna shujaa pasipo na maadui n
Najua hakuna ushindi pasipo na mapambano,
Siogopi mapambano, siogopi maneno siogopi masimango nataka kua shujaa
Najua dhahabu safi husafishwa kwa moto
Najua ushindi wangu utakuja nitashinda

Napenda kujifunza kwa tai, niliemfananisha na wewe
Tai hujenga nyumba yake juu ya maporomoko makali ambapo nyoka na hatari haziwezi kufika huko
Tai hujali makinda yake yakiwa madogo
(Tai) Ajengapo nyumba yake hujengea miti yenye miba mikali, juu yake hufunika manyoya lakini anajua nini anafanya
Ukifika wakati makinda yake yamekoma, taii huyanyima chakula yatoke ayafundishe kuruka
Yanapoendelea kukataa hupuliza manyoya
Miba alioweka huwalazimisha kutoka...
Lengo la tai si kuyaumiza makinda yake
Lengo la tai ni kuyafundisha kuruka juu
Yakitoka nje huyabeba mgongoni hupanda nayo juu kisha huyaachia,
Yanahangaika kutafuta mama yao, nguvu zao zikiisha mama yao hutokeza mbele
Kwa zoezi hilo hujifunza kuruka ndipo hugundua nia njema ya mama yao
Nawe Bwana Mungu nibebe kama tai nguvu zangu zikiisha nibebe kama tai
Nawe Bwana wangu nibebe kama tai nguvu zangu zikiisha nibebe kama tai
Lyrics copyright : legal lyrics licensed by Lyricfind.
No unauthorized reproduction of lyric.

Comments for Tangulia Mbele lyrics

Name/Nickname
Comment
Copyright © 2004-2024 NET VADOR - All rights reserved. www.paroles-musique.com/eng/
Member login

Log in or create an account...

Forgot your password ?
OR
REGISTER
Select in the following order :
1| symbol to the left of the suitcase
2| symbol to the left of the envelope
3| symbol at the bottom of the thumbs up
grid grid grid
grid grid grid
grid grid grid